Mkoa wa Tanga uko Kaskazini Mashariki mwa Tanzania na una eneo la kilometa za mraba 27,348. Ambazo zimegawanywa katika wilaya nane za Tanga, Muheza, Pangani, Korogwe, Lushoto, Handeni, Kilindi na Mkinga.
Hali ya hewa katika mkoa wa Tanga kwa ujumla ni ya joto ukiondoa eneo la milima ya Usambara ambalo linakuwa na hali ya baridi kwa kipindi kirefu. |