Mkoa una jumla ya viwanda 36 (Viwanda vikubwa na vya kati). Mwaka 2006 uzalishaji ulikuwa tani 980,543. Viwanda viliuza bidhaa ndani ya nchi kwa jumla ya tani 750,279 zenye thamani ya Sh. 134,683,242,383. Vile vile mauzo ya bidhaa nje ya nchi yalifikia tani 205,859 zenye thamani ya dola za Marekani 11,840,802. Bidhaa zilizouzwa kwa wingi ni zile za nyuzi (yarn); nyuzi za mkonge; kamba za mkonge; saruji, Chai vipodozi; sabuni za unga (Foma); minofu ya samaki na bidhaa za mbao.
Mwaka 2007, uzalishaji viwandani ulifikia tani 1,051,470. Bidhaa kiasi cha tani 774,201.4 zenye thamani ya Sh. 192.4 billioni ziliuzwa ndani ya nchi na mauzo ya nchi za nje yalifikia tani 622,097 zenye thamani ya Dola za Marekani 2,503,990,126. |