JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - OFISI YA WAZIRI MKUU - TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA      
tanga
 
     
 
     
ELIMU
 
Elimu [ Nyumbani ] au
 

ELIMU

 
Elimu Mkoa wa Tanga unasimamia elimu ya awali, elimu ya msingi na elimu yasekondari
Mkoa unashirikiana na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi katika kusimamia na kuendesha shughuli za elimu. Mkoa unatekeleza Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Sekondari (MMES 2004-2009). na Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM  II) baada ya MMEM I Kumaliza muda wake (2002- 2006)
 
 
ELIMU YA AWALI

Mkoa wa Tanga una jumla ya Shule za awali 483 zikiwemo za madarasa ya Serikali 850 na shule za awali zisizo za Serikali 12.  Idadi ya wanafunzi wanaosoma katika shule hizo ni 30,257 wakiwemo wavulana 16,395 na wasichana 13,862.

 
 
 
ELIMU YA MSINGI

Darasa la kwanza mwaka 2008 mkoa uliandikisha watoto 76,670.

Mkoa wa Tanga una jumla ya Shule za Msingi 920 mwaka 2008, kati ya hizo shule 853 ni za Serikali na 11 ni shule zisizo za Serikali. Wanafunzi wa shule za msingi ni 411,130 kati yao wavulana ni 211593 na wasichana ni 199537.

Mkoa wa Tanga una jumla ya walimu wa shule za Msingi 7017, kati yao 3514 ni wanaume na 3503 ni wanawake

 
IDADI YA SHULE ZA MSINGI KIWILAYA
 

Wilaya

Makadirio ya Idadi ya wa tu 2006

Idadi ya shule za msingi

Wastani wa idadi ya watu kwa shule

Idadi ya Vijiji /Mitaa

Wastani wa vijiji/ Mitaa kwa shule

Pangani

  45,885

31

1,480

      33

0.9

Muheza

294,326

106      

Mkinga

170

1,731

    175

1.0

Korogwe

272,956

159

1,717

    135

1.2

Tanga

261,613

91

767

      23

4.0

Handeni

280,927

142

2,103

    176

1.1

Kilindi

165,005

99

648

        64

1.3

Lushoto

437,379

218

2,006

     162

1.3

Total

        1,758,091

880

1,638

       714

1.3

 

Utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM)

 

MMEM I 2002 - 2006 ni mpango wa maendeleo wa Elimu ya Msingi ambao umejikita katika maeneo makuu

 

Mkoa umepata mafanikio makubwa kutokana na utekelezaji wa mpango wa Maendeleo ya elimu ya Msingi (MMEM). Idadi ya shule za Msingi imeongezeka kutoka shule 756 mwaka 2002 hadi shule 920 mwaka 2008. 

  1. Idadi ya vyumba vya madarasa (vya kudumu) imeongezeka kutoka 3,928 mwaka 2002 hadi 7,781 mwaka 2008.
  2. Nyumba za Waalimu zimeongezeka kutoka 706 mwaka 2002 hadi nyumba 2,490 mwaka 2008. 
  3. Aidha idadi ya Waalimu katika shule za msingi imeongezeka kutoka 6,172 mwaka 2002 hadi Waalimu 8,349 mwaka 2008

TAKWIMU ZA ELIMU YA MSINGI MKOA WA TANGA 2008

Aina ya Mahitaji

Mahitaji

Yaliyopo/zilizopo/Waliopo

Upungufu

Vyumba vya Madarasa

9,916

7,781

2,135

Nyumba za Walimu

10,556

2,490

8,060

Waalimu

10,283

8,329

1,954

Vyoo (matundu)

20,572

8,666

11,906

Madawati

181,400

139,924

41,553

 
MATOKEO YA MTIHANI WA ELIMU YA MSINGI MWAKA 2005

Mwaka 2007 wanafunzi waliosajiliwa kufanya mtihani wa cheti Elimu ya Msingi katika Mkoa wa Tanga walikuwa 41157, wakiwemo Wavulana 20,881 na Wasichana 20,276

Waliofanya mtihani walikuwa 39,760 kati yao Wavulana ni 20,188 na Wasichana ni 19,572 sawa na asilimia  98.2. Jumla ya wanafunzi 1,397 hawakufanya mtihani kati yao Wavulana ni 693 na Wasichana  ni 704 . Sababu za kutofanya mtihani ni utoro, mimba, ugonjwa na vifo.

Waliofaulu mtihani walikuwa 25,800 kati yao wavulana ni 14,002 na Wasichana ni 11,798 sawa na asilimia 63.8.

Jumla ya wanafunzi 25,476 wakiwemo wavulana 13,678 na wasichana 11,798 wamechaguliwa kujiunga  kidato cha kwanza mwaka 2008.  Idadi hii ni sawa na 98.7% ya watahiniwa wote 25,800 waliofaulu Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi (PSLE) mwaka 2007

Wanafunzi 324 sawa na (1%) ya waliofaulu wamekosa nafasi ya kuendelea na masomo ya Sekondari, kati yao Wavulana324 hakuna Wasichana waliokosa nafasi.

 

 
 
ELIMU YA SEKONDARI MKOA WA TANGA
 
Idadi ya Shule kwa kila Wilaya
Wilaya Idadi ya Shule
Shule za Serikali
Shule za Binafsi
Jumla
Handeni
20
1
21
Kilindi
11
11
Korogwe Mji
8
1
9
Korogwe Wilaya
24
1
25
Lushoto
56
9
65
Muheza
24
4
28
Mkinga
15
15
Pangani
5
1
6
Tanga
26
16
42
Jumla
189
33
222
 
TAKWIMU ZA ELIMU YA SEKONDARI MKOA WA TANGA 2008

Aina ya Mahitaji

Mahitaji

Yaliyopo/zilizopo/Waliopo

Upungufu

Vyumba vya Madarasa

     

Nyumba za Walimu

     

Waalimu

     

Vyoo (matundu)

     

Madawati

     
 

Utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Sekondari (MMES)

 
Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Sekondari MMES umejikita katika maeneo makuu yafuatayo
  1. Kuongeza upatikanaji wa Elimu ya Sekondari (Access)
    -Kupanua shule /Kujenga shule mpya ili kuongeza uandikishaji
    -Kupanua na kuboresha utoaji wa elimu ya sekondari kwa njia ya mfumo usio rasmi
  2. kutoa Elimu kwa Uwiano sawa (Equity)
    - kuboresha ushiriki wa wasichana, watoto wenye ulemavu, watoto wafugaji/ wawindaji
    -Kusaidia gharama za elimu kwa watoto yatima au watoto kutoka familia zenye kipato duni
    -Kuboresha miundo mbinu katika shule zenye ulemavu
  3. kuongeza ubora wa Elimu ya Sekondari (Quality)
    -Ajira za walimu
    -Kuzipatia shule ruzuku ya vifaa kwa kufundishia na kujifunza
  4. kuboresha Usimamizi na uendeshaji wa shule
 

Utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Sekondari ulianza mwaka 2005. Mkoa umepata mafanikio makubwa katika kutekeleza mapngo huu.

  1. Ongezeko la Shule za Sekondari -Mkoa ulikuwa na shule za Sekondari 104, kati ya hizo shule 73 za Serikali na shule 31 za Mashirika na sekta binafsi.  Mwaka 2008 Mkoa una shule za Sekondari 222, kati ya hizo shule 189 ni za Serikali na shule 33 ni za Mashirika na sekta binafsi.  Katika kipindi hiki, juhudi kubwa zimewekwa katika ujenzi wa shule za kutwa za Serikali ambapo kuanzia 2005 hadi Juni 2008 jumla ya shule 87 zimejengwa.
  2. Ongezeko la idadi ya wanafunzi wanaopata nafasi kuingia kidato cha kwanza katika shule za Sekondari za Serikali imekuwa kila mwaka.  Mwaka 2006 wanafunzi 13,030 walipata nafasi kuingia kidato cha Kwanza katika shule za Serikali.  Waliopata nafasi kuingia kidato cha kwanza katika shule za Serikali mwaka 2007 walikuwa 21,791 (au asilimia 92.39 ya waliofaulu mtihani 2006).
 
UCHAGUZI WA WANAFUNZI KUINGIA KIDATO CHA KWANZA 2008
Jumla ya wanafunzi 40,435 walifanya Mtihani wa Kumaliza elimu ya msingi mwaka 2007.  Waliofaulu mtihani huo ni wanafunzi 25,800 sawa na 63.8% ambapo Mkoa ulishika nafasi ya 5 Kitaifa.  Wanafunzi 25,544 wamechanguliwa kuingia kidato cha kwanza mwaka 2008. 
 
 
ELIMU YA SEKONDARI YA JUU (ADVANCED LEVEL)
mkoa wa Tanga unashule za sekondari za A-Level 13 kati ya hizo 5 ni za serikali na 8 za binafsi
 
 
Vyuo
Vyuo Vya Ualimu

Mkoa wa Tanga mwaka 2008 vipo Vyuo vya Ualimu vitano (5) na vingine viwili (2) vimepata vibali na ujenzi unaendelea.  Hii ni katika juhudi za kupata Walimu wa kutosheleza mahitaji katika shule za Msingi na shule za Sekondari. 

 
Vyuo Vya Vikuu

Mkoa una vyuo vikuu viwili ambavyo ni:

  1. Tawi la Chuo Kikuu Huria (Open University of Tanzania). 
  2. Chuo Kikuu cha Sebastian Kolowa – ambacho kimeanzishwa 2007 Wilayani Lushoto chini ya Kanisa la Kilutheri.

 

 
Vyuo Vya Vingine
  1. Vyuo vya Afya: Mkoa unavyuo vya Afya-Nurses Training Centre – Tanga na Vector Control Training Centre Muheza
  2. Vyuo vya ufundi VETA:
 
ELIMU YA WALEMAVU (SPECIAL – EDUCATION):
 

Wataalam wanasema ulemavu ni sehemu ya maisha katika jamii. Kitaalam10%, katika jamii ni walemavu. Ulemavu unaweza ukazaliwa nao au ukakukuta ukubwani. Watu wenye ulemavu ni sawa kabisa na watu wengine mbele za Mwenyezi Mungu. Hivyo wao pia wana haki ya kupata Elimu kama watu wengine na ulemavu uko wa aina nyingi.

Watoto wenye  ulemavu kama wasioona wanahitaji nyenzo tofauti katika tendo la kujifunza. Mkoa wetu una shule tatu tu za walemavu nazo ni Irente (Lushoto), pongwe na Masiwani (Tanga Jiji). Mbili ni za watoto wasioona na moja ni ya watoto wenye akili taahira na utindio wa ubongo.

Wazazi wenye watoto wenye ulemavu hawapendi kuwapeleka watoto wao shuleni. Wengi wao wanaona aibu na wanafikiri ulemavu ni kama Laana kuwa na mtoto wa aina hiyo.

Elimu ya walemavu ni gharama sana. Hivyo mara hyingi huendeshwa kwa gharama za wahisani au wafadhili (km. Irente inaendeshwa na K.K.K.T. na Masiwani ni Wafinland ambao wanasaidia.

Wataalam wa elimu Maalum ya Walemavu walimu ni wachache sana na kuwasomesha pia ni gharama

 

 
MASUALA MTAMBUKO (CROSS-CUTTING ISSUES)

Ukimwi

Katika harakati za kupambana na Ukimwi, elimu dhidi ya Ukimwi hutolewa kwa shule zote za Halmashauri za Mkoa wa Tanga kupitia somo la EDU. Pia kuna uelimishaji rika Kwa ujumla wananchi wanaelewa athari za ugonjwa wa UKIMWI na viongozi wameweka azimio kwamba katika kila Kikao lazima suala la UKIMWI lizungumziwe
 

Jinsia

Masuala ya jinsia watu wameyaelewa katika Mkoa wa Tanga kutokana na ushirikishwaji wa Mpango wa Hifadhi na Maendeleo ya mwambao wa Mkoa wa Tanga. Mpango wa Elimu Dhidi ya UKIMWI (EDU) - MEUSTA  wanatoa elimu kwa jamii kuhusu usawa wa jinsia. Wanawake wanashirikishwa kwenye Kamati za shule, Bodi za Shule na maendeleo ya shule kwa ujumla
 

Mazingira

Katika suala zima la kuhifadhi Mazingira, Shule za msingi zimeanza kuweka uzio katika maeneo yao ya Shule, kupanda miti na bustani za maua.  Ili kuzuia uharibifu wa mazingira katika vijiji vilivyo na shule kumeundwa kamati mbalimbali za kuzuia majanga kama moto n.k. Pia mpango wa Hifadhi na maendeleo ya mwambao wa Mkoa wa Tanga umeanzisha Elimu ya Mazingira ya Mwambao katika Shule za Msingi kwa Jiji la Tanga, Halmashauri ya Pangani na Muheza
 
ELIMU YA WATU WAZIMA

Kufuatana sensa ya mwaka 2002 inaonesha kuwa katika Mkoa wa Tanga kati ya watu 1115449 wenye umri wa miaka zaidi miaka kumi   832102 wanajua kusoma, kuhesabu na kuandika sawa na asilimia 74.6%, na katika hawa asilimia 51.5% ni wanaume na 48.5 ni wanawake, kwa takwimu hizi watu wasiofuta ujinga wa kutojua KKK ni 283347 sawa na asilimia 25.4%.

 Mkoa umedhamiria kuchukua hatua madhubuti ya kufuta ujinga kama ifuatavyo:-

  • Kufufua Kamati za Elimu ya Watu Wazima za Wilaya ili zianze kufanya kazi.

 

  • Halmashauri kuboresha  mazingira ya kufundishia na kusomea  watu wazima.
  • Kuimarisha Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi kwa walioikosa (MEMKWA).

Halmashauri kuboresha utoaji wa fedha za posho (Honoraria) kwa wawezeshaji wa Kisomo. na MEMKWA

 
ELIMU YA KUJIENDELEZA
Chuo Kikuu Huria
Tunacho kituo kimoja katika Mkoa  ambacho kimefunguliwa mwaka 2000 na hadi hivi sasa wanaoendelea na masomo mbalimbali ni wanaume 464 na wanawake 145 jumla wote wanachuo ni 609 na wanachuo ambao wamekwisha hitimu ni wanaume 13 na wanawake 6 jumla 19 katika shahada za BA Education  BSC Education, BCOM,  LLB na CYP
 
Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima

Katika Mkoa tunacho kituo kimoja ambacho kinaendesha masomo ya kujiendeleza kwa watahiniwa wa Kidato cha IV. Yapo madarasa matatu mjini Tanga katika vituo vitatu vya Eckernforde, VETA na Chumbageni,   vyenye jumla ya wanafunzi 299 wakiwemo wanaume 117 na wanawake 182.

 
MATATIZO YA ELIMU  MKOANI
  1. Upungufu mkubwa  wa walimu wa shule za sekondari hasa kwenye shule mpya tulizofungua kwa masomo ya Sayansi, Hisabati na Sanaa. 
  2. Upo uhaba wa vifaa vya elimu kwa wanafunzi walemavu – wasioona, taahira na wenye mtindio wa ubongo.
  3. Madai ya walimu ambayo yalihakikiwa  wakati wa Tume ya Waziri Mkuu mwaka 2004.  Walimu Mkoani walikuwa wanadai kiasi cha  Shs.844,597,888/36 kwa ajili ya uhamisho, matibabu, masomoni nk.  Hadi sasa wamelipwa Shs.602,618,804/=  sawa na asilimia 71.4%.   Walimu bado wanadai kulipwa Shs.151,515,210/96.
  4. Kasi ya ujenzi wa shule za sekondari za kutwa zinazaotarajiwa kufunguliwa Machi 2006 bado siyo kubwa sana kwa kukosa  fedha za kuchangia kwa upande wa wananchi kwa sababu ya upungufu wa chakula katika maeneo mengi.
 
 
Elimu [ Nyumbani ] au
 
     
Copyright © 2008 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Box 5095 Tanga, TEL: 027 - 2642430, FAX: 027-2647752