JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - OFISI YA WAZIRI MKUU - TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA      
tanga
 
     
 
     
TAARIFA ZA FEDHA NA BAJETI
 
[ Taarifa za fedha ] Bajeti [ Nyumbani ] au
 

MPANGO NA BAJETI YA MATUMIZI KWA MWAKA 2008/2009 MKOA WA TANGA

 
Mapendekezo ya Mpango na bajeti ya matumizi ya kawaida na shughuli za maendeleo kwa mwaka 2008/2009 yametayarishwa yakiwa na madhumuni ya kuendeleza utekelezaji wa  malengo ya Mkakati wa Taifa wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini (MKUKUTA) na malengo ya Millenia(Millenium Development Goals).
Mr R. S. Kakunya
Mchumi Mkuu -Sekretarieti ya Mkoa
 

Pia mpango na bajeti ya 2008/2009 una nia ya kukamilisha  utekelezaji  wa malengo ya Mpango Mkakati wa Sekretariati ya Mkoa kwa kipindi cha 2005/06 – 2008/2009 (R.S Medium Term Strategic Plan 2005 – 2008) na kuendeleza utekelezaji wa malengo ya Mipango Mkakati ya Serikali za Mitaa.  Aidha Mpango huu ni wa tatu katika jitihada za kutekeleza malengo ya Ilani ya Uchaguzi Mkuu ya CCM (2005) kipindi cha 2005 hadi 2010.

Mpango  Mkakati wa Mkoa ulitayarishwa Februari 2005 kwa kushirikisha viongozi, na watendaji katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, ofisi za wakuu wa wilaya na wadau wengine muhimu ikiwa ni pamoja na Serikali za Mitaa.  Malengo makuu (key Result Areas) ya Mpango Mkakati wa Sekretariati ya Mkoa ni:

  • Kuimarisha ufanisi katika utendaji kazi kwa viongozi na watumishi.
  • Kuboresha mazingira ya kufanyia kazi katika ofisi za mkoa, wilaya hadi ngazi ya tarafa.
  • Kuhakikisha utawala bora katika mkoa unadumishwa na kuendelezwa.
  • Kujenga na kuendeleza uwezo wa viongozi na watendaji  katika utekelezaji wa shughuli za maendeleo na utoaji huduma katika Serikali za Mitaa.
  • Kuhakikisha kuwa Serikali za Mitaa zinatoa huduma bora kwa wananchi na Utawala bora unadumishwa.
  • Kuhakikisha kuwa masuala mtambuka – hasa janga la ukimwi, usawa wa kijinsia na hifadhi ya mazingira vinapewa kipaumbele na kushughulikiwa katika serikali za mitaa, kila taasisi, vikundi vya kijamii na wananchi kwa ujumla.
 
Mambo yaliyozingatiwa katika kuandaa na kuchambua mipango na bajeti

Mambo yaliyozingatiwa katika kuandaa na kuchambua mipango na bajeti ni pamoja na

  • Mwongozo uliotolewa na Wizara ya Fedha na Uchumi “Guideline for the Preparation of Medium Term Plan and Budget Framework for 2008/09 – 2010/2011.”  Pamoja na viwango vya bajeti (Budget Ceilings) vilivyowekwa kwa mwaka 2008/2009.
  • Sera za sekta mbali mbali- Sera za Afya, Maliasili- Misitu, Mazingira, Maendeleo ya Jamii na Sera ya Uboreshaji wa Serikali za Mitaa (Local Government Reform) sera ya Maendeleo Vijijini, mkakati wa kukuza uchumi na  kupunguza umaskini (MKUKUTA), nk.
  • Mipango ya muda wa kati iliyoandaliwa kwa kuzingatia Dira ya Taifa (Vision 2025) na maazimio ya vikao vya Mkoa na Wilaya (k.m. Agizo la Mkonge, Mipango ya Halmashauri) na Malengo ya Programu ya Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi (2005 - 2010), Malengo ya Programu ya Milenia 2015, Mpango Mkakati wa Mkoa (SP) uliopitishwa 2005, nk.
  • Hali ya Maendeleo iliyofikiwa hadi sasa, matatizo na mafanikio katika Wilaya (Current Development Status, Opportunities and Obstacles to Development).  Uendeshaji wa Wilaya mpya ya Mkinga.
  • Hali ya uchumi wa Taifa hasa kwa kuzingatia mafanikio na matatizo ya utekelezaji wa bajeti ya 2007/08; mwelekeo wa Bajeti ya Taifa kwa mwaka 2008/09 na matatizo yanayotarajiwa kujitokeza (k.m. ukame na upungufu wa chakula).
 
MALENGO YA MWAKA 2008/2009
 

Katika mwaka 2008/2009 Mkoa umepanga kutekeleza malengo yafuatayo:

  • Kujenga uwezo wa Serikali za mitaa kwa kutoa ushauri, na mafunzo kwa wataalam n.k.
  • Kutoa ushauri wa kitaalam kwenye Serikali za Mitaa kuhusu masuala ya Menejimenti, utawala, uzalishaji mali, huduma za kiuchumi na huduma za jamii.
  • Kuimarisha utawala bora katika mkoa na kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji.
  • Kuimarisha uwezo wa wataalam na viongozi katika utendaji na usimamizi wa kazi.
  • Kushughulikia masuala mtambuka (cross-cutting issues)  hasa vita dhidi ya rushwa, kudhibiti kuenea kwa UKIMWI, kuendeleza usawa wa kijinsia na kuhifadhi mazingira.
  • Kuratibu na kusimamia utekelezaji wa shughuli za maendeleo, na utoaji wa huduma katika Halmashauri na Mkoa kwa jumla.
  • Kutekeleza miradi ya kimkoa, na kufuatilia na kutathmini utekelezaji wa miradi na programu za maendeleo ya sekta mbalimbali katika Halmashauri.
  • Kuratibu programu ya uboreshaji wa Serikali za Mitaa.
  • Kuendelea kutoa huduma za tiba na kinga katika hospitali ya Mkoa.
  • Kusimamia na kufuatilia utekelezaji wa miongozo, sera za Serikali Kuu katika Serikali za Mitaa na kutoa taarifa mbalimbali zinazohitajika.
  • Kusimamia matumizi ya fedha za  ruzuku au misaada zinazotolewa kwa Serikali za Mitaa kutoka Serikali Kuu.
 
   
MUHTASARI WA MAKADIRIO KWA MWAKA 2008/2009:
 

Ili kutekeleza shughuli zilizopangwa kufanyika mwaka 2008/2009, Mkoa uliomba kuidhinishiwa jumla ya shs. 74,080,170,224  kama ifuatavyo:

 
Bajeti kwa Matumizi ya Kawaida
 

Mwaka 2008/2009 Mkoa unapendekeza  kutumia Tshs. 54,745,625,224 kwa ajili ya uendeshaji wa shughuli za kawaida za Serikali. 
Serikali Kuu itatumia Tshs. 5,145,570,396 na Ruzuku kwa Serikali za Mitaa ni Tshs. 49,600,054,828.
Kati ya fedha hizo; Tshs. 42,765,658,224 ni makadirio ya Mishahara (P.E) na Tshs. 11,979,967,000  ni bajeti ya matumizi mengineyo (O.C.).

 
PROGRAMU/ MIRADI YA MAENDELEO ITAKAYOTEKELEZWA KWA BAJETI YA 2008/2009
 

Kiasi cha Tsh. 19,334,545,000/=/= kimeombwa kitumike kwa utekelezaji wa miradi ya Maendeleo.  Kati ya fedha hizo Fedha za hapa (Local funds ) Tsh.  2,080,167,000/= na Fedha za nje ni Tsh. 17,254,378,000/= .

Miradi chini ya Sekretariet ya Mkoa itatumia Jumla Shilingi 1,465,347,000 ambazo Fedha za hapa (Local 1,076,217,000 na Fedha za nje (Foreign) 389,130,000,000

Kufuatia lengo la Serikali la kupeleka madaraka na rasilimali zaidi kwa wananchi (Decentralization by Devolution); mwaka 2008/09 Serikali za Mitaa zitatekeleza Programu/Miradi mbali mbali ambazo zimtengewa Jumla ya Tshs 17,869,198,000 ambazo Fedha za hapa (Local)  Tshs 1,003,950,000 na Fedha za nje (Foreign) Tshs 16,865,248,000

 
MIRADI CHINI YA SEKTRETARIET YA MKOA
 
Mradi Makadirio
Ujenzi wa Ofisi ya DC Pangani
450,000,000
Ujenzi wa nyumba ya Katibu Tawala – Pangani                     
90,000,000
Ukarabati majengo ya Serikali
50,000,000

Ukarabati Ofisi za Wakuu wa Wilaya

60,000,000

Ukarabati nyumba za Wakuu wa Wilaya Tanga, Handeni na Lushoto

160,000,000

Uimarishaji Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

90,217,000
Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
70,000,000
Mfuko wa Afya ya Jamii (Health Basket Fund na Health Sector Global  Fund na HIV/AIDS)
310,000,000
   
 
 
 
MIRADI YA HALMASHAURI
 
Kufuatia lengo la Serikali la kupeleka madaraka na rasilimali zaidi kwa wananchi (Decentralization by Devolution); mwaka 2008/09 Serikali za Mitaa zitatekeleza Programu/Miradi mbali mbali kama ifuatavyo
 
Mradi/ Program Makisio (Tshs)
Programu ya kutoa ruzuku ya Maendeleo (Local Government Capital Development Programme)
3,217,993,000
Programu ya ujenzi wa Barabara (Local Government Road Network (LGTP/VTTP)
1,748,000,000
Programu ya Uendelezaji Kilimo (Agricultural Sector Dev. Programme)- Basket Fund
3,599,788,000
Programu ya Hifadhi Misitu (Participatory Forest Management (Finland)
546,417,000
Programu ya Maendeleo mijini na usimamizi wa mazingira (Urban Dev. And Environmental Management) -Denmark
304,893,000
Programu ya Uendelezaji Maji Vijijini (Rural Water Supply and Sanitation) -ADF
3,369,418,000
Programu ya Uboreshaji Huduma za Afya (Health Service Basket Fund)
2,422,088,000
Mfuko wa Afya ya Jamii (Health Sector Global Fund)
1,100,000,000
Miradi mingine ya Halmashauri
1,003,950,000
 
     
    Bonyeza Hapa Kusoma Zaidi >>
     
     
    [ Taarifa za fedha ] Bajeti [ Nyumbani ] au
    Rudi juu
     
         
    Copyright © 2008 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Box 5095 Tanga, TEL: 027 - 2642430, FAX: 027-2647752