JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - OFISI YA WAZIRI MKUU - TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA      
tanga
 
     
 
     
Kamati ya Bunge ya Fedha Serikali za Mitaa
 
kamati ya fedha [ Nyumbani ] au
 

Kikao cha Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa mkoani Tanga

kikao kimepitia matumizi ya Fedha za Serikali za Mitaa za mwaka wa Fedha 2006/2007 kilichofanyika Wilayani Lushoto. Kamati ilipokea taarifa za Mapato na Matumizi ya fedha kwa Halmashauri za Wilaya Pangani, Mkinga, Korogwe, Handeni, Kilindi, Lushoto na Muheza, Halmashauri ya Mji Korogwe na Halmashauri ya Jiji la Tanga

Kamati ilipata fursa kukagua miradi ya Maendeleo ilyotekelezwa katika mwaka wa fedha 2006/2007 kwa Halmashauri zote za Mkoa wa Tanga kuanzia tarehe 22 -25 mwezi oktoba, 2008. ukaguzi wa miradi ulimaziwa kwa kiako cha majumuisho kilichofanyika ukumbi wa Mikutano Halmashauri ya wilaya ya Korogwe tarehe 26 Oktoba, 2008

 
baada ya kupokea taarifa za Halmashauri zote. Kamati ilitoa maagizo mbalimbali ambayo watendaji wa Halmashauri wanatakiwa wayatekeleze katika kipindi cha Miezi mitatu
 
Wajumbe wa Kamati ya Fedha waliohudhuria kikao Wilayani Lushoto Mkoani Tanga
  1. Mhe. Mgana Msindai (Mb)-Makamu Mwenyekiti wa Kamati
  2. Mhe. Mchemba (Mb)
  3. Mhe. Chaurembo (Mb)
  4. Mhe. Malangalila (Mb)
  5. Mhe. Iddi Azzan (Mb)
  6. Mhe. Eng Mhina (Mb)
  7. Mhe. Simbachawene (Mb)
  8. Mhe. Kiwelu (Mb)
  9. Mhe. Mabina (Mb)
  10. Bw. Kileo - Katibu wa Kamati
 
 
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Fedha na Utawala Mh Mgana Msindai (Mb) akitoa majumuisho ya ziara ya Kamati Mkoani Tanga Oktoba 25 2008 katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya Korogwe, Mkoani Tanga
Watendaji na Wasimamizi wa Halmashuri wakimsikiliza Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Fedha na Utawala Mh Mgana Msindai (Mb) akitoa majumuisho ya ziara ya Kamati Mkoani Tanga Oktoba 25 2008 katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya Korogwe, Mkoani Tanga
 

Maagizo ya Kikao cha Kamati ya Fedha

 

Maagizo yaliyotolewa kwa Halmashauri zote kwa ujumla ni yafuatayo

 
  1. Halmashauri zimeonekana Makusanyo yao ya Mapato ya fedha za ya ndani (Own Source Fund )yako chini sana hivyo mikakati iwekwe kuweza kuboresha ukusanyaji wa mapato ili kufikia/ kuvuka kiwango kilichowekwa kwa kila Halmashauri.
  2. uwezo wa kujitegemea ni 2% Halmashauri zinategemea sana fedha toka serikali kuu. Wenyeviti wasimamie suala zima la ukusanyaji mapato ya ndani.
  3. Fedha za Ruzuku ya kuwajengea uwezo (Capacity building Grants) zitumike kuwasomesha walimu na wenyeviti wa vijiji ili kuwajengea uwezo wa kuweza kutekelza majukumu yao.
  4. Utekelezaji wa Miradi mingi hauoneshi nguvu za wananchi. Halmashauri ionyeshe nguvu za wananchi katika utekelzaji wa kila mradi kwenye taarifa za mtaumizi ya fedha
  5. Uibuaji wa miradi ya TASAF bado ni mdogo, hivyo miradi mingi ya TASAF iibuliwe na kupelekwa ofisi ya TASAF na wawape nakala wabunge wawasaidie kufuatilia
  6. Fedha nyingi za Miradi zinabaki bila kutekeleza miradi kwa kipindi kilichopangwa. Halmashuri wahakikishe fedha zinatumika na miradi inatekelezwa kama ilivyopngwa
  7. Halmashauri zenye Mamlaka za miji hazitengi fedha na kuzipeleka katika mamlaka, fedha zitengwe na zipelekwe Mamlaka ya Miji midogo kama mpango unavyoonyesha
  8. Fedha za wanafunzi za "capitation" walizopekea mashuleni ni pungufu, tofauti ya fedha hizo kwa kila Halmashauri ikamishe na kuzipeleka kwa wanafunzi
  9. Madiwani wasimamie 20% ya fedhaza Fidia za vijiji zipelekwe vijijini kwa kila Halmashauri
 
Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo
 

Wajumbe wa kamati ya Bunge ya Fedha za Serikali za Mitaa walikagua miradi katika Halmashauri za Mkoa wa Tanga ambazo ni Halmashauri ya Jiji la Tanga, Halmashauri ya Mji Korogwe, Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe, Mkinga, Muheza, Pangani, Handeni, Kilindi na Lushoto kuanzia tarehe 22 mpaka 24 mwezi Oktoba mwaka 2008.

Wajumbe walitembelea miradi mingi ya jamii ikiwa ni miradi ya Maji chini ya Mpango wa Maji Quick wins, Miradi ya Afya (Health basket Fund), Miradi ya Kilimo (ASDP na PADEP), Miradi ya Elimu (MMES), Miradi ya Programmu ya Kusaidia Halmashauri (LGCDG), Miradi ya Barabara (Road Fund), Miradi ya Maliasili (Participatory Forest Management )Miradi ya Jamii chini ya TASAF na minigine Mingi

 
Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Fedha na Utawala Mh. Iddi Azzan (MB) aliyeshika Pump na Mh. Eng Mhina (MB) wanne kutoka kushoto wakikagua Mradi wa Maji kijiji cha Kibambani Manza Wilayani Mkinga Mkoani Tanga 24 Oktoba 2008
 
 
Maagizo ya Kamati ya Bunge ya Fedha za Serikali za Mitaa baada ya ukaguzi wa Miradi
 
  1. kuna maeneo ambayo hatujawa "serious" katika kutekeleza wajibu wetu wa kuwaletea wananchi maendeleo
  2. Serikali imewaamini Wakurugenzi, Waheshimiwa Madiwani ndio maana wakachaguliwa kazi za Mstahiki Meya na Wanyeviti ni kusimamia maendeleo Waheshimiwa mkilegalega hatuwatendei haki wananchi. Kazi za watendaji tuwaachie watendaji. Mkurugenzi na Mkuu wa Idara wanaofanya vibaya washughulikie hapo hapo
  3. Makandarasi wabovu wasipewe kazi na Zabuni zinazopitishwa Madiwani wapewe nakala kwa ufuatiliaji
  4. Madiwani wakague miradi kila robo ya mwaka. Wakurugenzi wasiwe kikwazo
  5. Viporo vyote vya Miradi ya mwaka 2006/07 na 2007/08 ni kazi ya Halmashauri kwenda kumalizia, Wananchi wameshafanya kazi yao
  6. Vipaumbele vya kila Wilaya vipewe umuhimu katika kuvitekeleza
  7. Yote yaliyojadiliwa kwenye kikao cha LAAC na majumuisho Madiwani wapewe taarifa
  8. Kuna upungufu mkubwa wa walimu katika shule za Sekondari, ni tatizo la kitaifa taarifa iandaliwe kwa kila Halmashauri

 

Baada ya kuitoa majumuisho mwenyekiti msaidizi wa kamati hiyo aliwashukuru viongozi na watendaji wa Halmashauri na Mkoa kwa ushirikiano wao ambao uliwezesha kazi yao kukamilika.
 
Serikali za mitaa [ Nyumbani ] au
Rudi juu  
 
     
Copyright © 2008 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Box 5095 Tanga, TEL: 027 - 2642430, FAX: 027-2647752