JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - OFISI YA WAZIRI MKUU - TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA      
tanga
 
     
 
     
UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO KWA MWAKA FEDHA 2007/2008
 
[ Nyumbani ] au
 
Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo ya mwaka wa fedha 2007/2008 iliyotekelezwa katika Halmashauri za Mkoa wa Tanga, ulianza tarehe 6 - 28/11/2008.  Lengo kuu la ukaguzi wa miradi hii lilikuwa ni kuona utekelezaji halisi na thamani ya fedha kwa kila mradi. Aidha timu ziligawanyika katika makundi 4 na zilihusisha wataalamu kutoka ngazi ya Mkoa na Halmashauri ili kupata uzoefu/kujifunza katika maeneo mengine ndani ya Mkoa kama ilivyoagizwa na kamati ya Bunge ya Fedha na Utawala

Katika ukaguzi huo timu zilikutana na uongozi wa Halmashauri na kupata taarifa fupi ya utekelezaji wa miradi kwa mwaka wa fedha 2007/08. Baada ya kupata taarifa hiyo timu zilichagua miradi  katika maeneo mbalimbali.

Aidha jumla ya miradi 104 ilikaguliwa yenye thamani ya shilingi xxxx katika maeneo mbalimbali ya Halmashauri za mkoa wa Tanga.

 
 
HALMASHAURI YA WILAYA YA PANGANI

Wilaya ya Pangani jumla ya miradi 15 ilikaguliwa yenye thamani ya shilingi 345,259,099 ambapo jumla ya shilingi 265,259,099 zimetumika.

Hali ya Miradi mingi inaridhisha hasa utekelezaji wa Miradi ya Maji unaenda vizuri sana. Msisitizo ni miradi inayohusisha wannchi ambao uchangiaji wao umekua ni mdogo.

 

Utekelezaji

Hali ya miradi ilikaguliwa na utekelezaji wake na hatua ilifiyofikia imeonyeshwa kwenye jedwali lifuatalo
 
 
 
NA
MRADI
FEDHA ILIYOTENGWA
FEDHA ILIYOTUMIKA
MAELEZO YA MRADI
1 Ujenzi wa vituo vya kukusanyia maziwa wa chama cha ushirika (WAWAPA). 40,000,000 25,000,000

jengo liko kwenye linta. Halmashuri idara ya ushirika wasimamie ukamilishwaji wa mradi

2 Ujenzi wa Ofisi ya Kata Pangani magharibi 14,000,000 6,000,000 Vyumba 8 vimejengwa viko kwenye linta. Halmashauri imfuatilie Mkandarasi amalizie.
3 Ujenzi kituoo cha Uhamilishaji AI 36,000,000 16,000,000 Jengo liko usawa wa Linta. Mradi usimamiwe ukamilike kwa ratiba
4 Ujenzi wa Nyumba ya Mkurugenzi wa Wilaya 50,000,000 26,000,000 Jengo liko kwenye mtambaa panya. Fedha iliyotengwa inaweza kupungua
5 Ukarabati mradi wa Maji Kimang’a

63,000,000 (ADB 60M, Wilaya 3M)

Umekamilika Mambomba yamelazwa urefu wa km. 7 kutoka Boza (pumping station), tanki la maji lenye ujazo wa lita 23,000 limefanyiwa ukarabati na kupaka rangi na kuweka vituo 3 vya kuchotea maji
6 Ujenzi wa nyumba ya Mganga Kigurusimba Madanga 22,050,400/ TASAF Imekamilika Ujenzi wa jengo na thamani ya fedha imeonekana
7 Ukarabati wa mradi wa maji Mkalamo 33,448,000 Ukarabati wa tanki la maji umefanyika, injini mpya imewekwa, uzio wa seng’eng’e umewekwa, vituo vya kuchotea maji 6 vimejengwa na mabomba yamelazwa.
8 Ujenzi wa vyumba 2 vya madarasa na nyumba 2 za waalimu 13,400,000 Haijakamilika Ushiriki wa wananchi ni mdogo katika ujenzi wa madarasa na nyumba za waalimu. Fedha za Capitation zinatumika katika ujenzi tofauti na malengo yake. Ujenzi wa madarasa haupo katika kiwango kinachostahili.
9 Ujenzi wa mradi wa Soko Mkalamo chini ya Mkandarasi Bullem Investment. 20,000,000 7,000,000 Msingi umekamilika.
Thamani ya fedha iliyolipwa hailingani na kazi iliyotekelezwa. Utekelezaji wa mradi unakwenda taratibu
10 Ukarabati wa kituo cha Afya Mwera 3,641,360 joint rehabilitation fund umekamilika Usimamizi ulikuwa mzuri na thamani ya fedha imeonekana
11 Ujenzi wa vyumba 3 vya darasa Mwera Sekondari 24,000,000
(CDG)
Sakafu imeanza kubomoka, mbao zilizotuka kupaua ni laini (soft wood), madirisha hayajawekwa nyavu, madarasa 2 hayana zege kwa ajili ya sakafu
12 Ukarabati wa mradi wa maji Mwera 23,419,339
Quick wins.
umekamilika Ununuzi wa kiwanja, mota mpya, ujenzi wa tanki umefanyika, ukarabati wa vituo 2, kulaza bomba na kufunga bomba za kuingiza na kutoa maji kwenye tanki, kuweka uzio kuzunguka eneo la tanki
13 Ukarabati wa barabara ya Bwenimseko   umekamilika Uwepo mipango ya muda mrefu ya kuinusuru barabara hiyo isiharibiwe na maji ya bahari
14 Ujenzi wa Kizimba cha taka ngumu Mjini 500,000 (CDG) Umekamilika Mhandisi Ujenzi aandae ramani za ujenzi wa vizimba vyenye ubora na kukidhi mahitaji ya Mji.
15 Ujenzi wa choo cha umma sokoni 1,800,000 1,800,000 Shimo la urefu wa m16 limechimbwa, vyoo matundu 5 yamechimbwa na kuta za choo zimepandishwa kwa ngazi 4 na fedha zilizotengwa zimekwisha
 
HALMASHAURI YA JIJI LA TANGA
 

Wilaya ya Pangani jumla ya miradi 13 ilikaguliwa yenye thamani ya shilingi 179,643,278 ambapo jumla ya shilingi 164,740,819 zimetumika.

Hali ya Miradi mingi inaridhisha utekelezaji wake. Msisitizo ni miradi inayohusisha ujenzi mara nyingi imekuwa haisimamiwi kwa karibu na Mhandisi wa Ujenzi. Utekelzaji wake unakua chini ya kiwango

 
 
NA
MRADI
FEDHA ILIYOTENGWA
FEDHA ILIYOTUMIKA
MAELEZO YA MRADI
1
    Ujenzi wa nyumba ya mganga katika kituo cha Afya Mikanjuni
15,000,000  

Ujenzi haukufuata taratibu wala haukuzingatia mkataba. Baadhi ya kuta zimeanza kupasuka kabla ya mradi kukamilika.
Mkandarasi arekebishe na kukamilisha kazi Vinginevyo Mkandarasi asilipwe “retention” baada ya kukamilisha kazi

2
    Ujenzi wa madarasa manne Mikanjuni Sekondari

14,959,159
“CDG”

  vyumba vilivyokamilika ni 2 sio 4 kama taairfa ilivyosema.
Taarifa zitolewe kwa usahihi, na madarasa yanatakiwa yakamilike kabla ya Januari 2009
3
    Ujenzi wa ofisi ya Kata Mwanzange
6,767,280
CDG
  Jengo liko usawa wa Madirisha
Utekelezaji wake unakwenda taratibu
4 Ujenzi wa madarasa 6 Sekondari ya Toledo 20,230,247
CDG
  Madarasa 2 yamekamilika. Madarasa 4 yamepauliwa. Madarsa yakamilishwe kabla ya Januari 2009
5 Uujenzi wa madarasa 5 Sekondari ya Maweni 8.439,484
CDG
umekamilika Upauaji wa vyumba vilivyojengwa hauko katika viwango
Mhandisi ujenzi kuhakiki hatua za utekelezaji wa mradi
6 Ujenzi wa madarasa 4 Sekondari ya Nguvumali 14,959,159 15,856,700 Vyumba 2 vimejengwa tofauti na mpango ujenzi wa 4
Maradasa mawili yaliyobakia yajengwe kama mpango ulivyokuwa.
7
    Ujenzi wa madarasa 3 Sekondari Chumbageni
13,211,977   Vyumba 3 vimejengwa. Bado ceiling board na rangi
Kamati imeridhishwa Sehemu zilizobaki zimaliziwe
8
    Ujenzi wa ofisi ya Kata Central
5,334,835   Jengo limefikia usawa wa lenta na fedha zimekwisha
Halmashauri itafute fedha za kumalizia ujenzi
9 Kuboresha bustani za Jiji

20,000,000 (UDEM)

4,200,000 kamati Haukuridhwa na Kazi ya kuboresha bustani.
Jiji liongeze kasi ya ukarabati ili kazi zimalizike kwa wakati
10
    Ujenzi wa vyoo matundu 20 vya VIP
13,022,000   Vyoo matundu 10 vimejengwa na kugharimu kiasi cha Tshs. 9,586,000/= vipo katika hatua ya umaliziaji
11
    Ujenzi wa ofisi ya kata Makorora
15,449,137 4,000,000 Ujenzi wa ofisi upo katika hatua za umaliziaji
Kamati imeridhika na utendaji kazi na hatua zilizofikiwa
12
    Mradi wa uzalishaji wa kuku wa kisasa kikundi cha Juhudi Mabokweni
23,500,000 23,500,000

Ramani iliyotumika katika ujenzi ni tofauti na iliyoandaliwa kutokana na makisio ya Mhandisi. Jengo lina nyufa na umaliziaji bado kukamilika.

13 Matengenezo ya kawaida ya barabara km. 10.4 ya Chongoleani - Mwanyungu na Mpirani 8,770,000 8,770,000 Matengenezo yamefanyika kama ilivyopangwa.
Kalavati linahitajika kuwekwa katika barabara sehemu inayokaribia kuingia kijijini Chongoleani
HALMASHAURI YA WILAYA YA MKINGA
 

Katika maeneo ya Mwambao; Duga, Moa n.k, suala la uchangiaji bado linahitaji hamasa kubwa sana. Wakati wa zoezi la ukaguzi, wananchi au kupitia kamati za shule au kamati ya ujenzi, baadhi yao hawaoni umuhimu wa kuchangia ujenzi wa madarasa au nyumba za walimu. Timu ya ukaguzi ya sekretarieti ya mkoa pamoja na wataalamu kutoka Halmashauri ya Mkinga, waliweza kushauri jinsi ya kuchangia kama ifuatavyo:

  1. Wananchi kama hawana fedha, wachangie kwa mfumo wa kutumia rasilimali walizonazo ili zigeuzwe kwua fedha; mfano kutoa nazi, kuku, n.k. je ni wangapoi watakubaliana na dhani hii?
  2. Licha cha kuiticha vikao vya kujadili maendeleo yao, wananchi bado wanasita na kutoa visingizio vya kuilaumu Serikali.  Mwenyekiti wa Kijiji na Mtendaji wa Kata pamoja na Kamati za shure zione umuhimu wa kujadili kila mara.
 
NA
MRADI
FEDHA ILIYOTENGWA
FEDHA ILIYOTUMIKA
MAELEZO YA MRADI
1
    Ujenzi wa nyumba ya mwalimu katika shule ya msingi Manza
3,600,000 3,927,000

2,537,500 zinahitajika kumalizia jengoU
Juhudi ya ziada ifanyike kuwahamasisha wananchi kuchangia nguvu zao.

2 Ukarabati wa barabara ya Zingibari hadi Mbuluni km.9.0 14,650,000  

Katika bajeti ijayo itengwe fedha kumalizia km 3 zilizorukwa na kukarabati sehemu zilizoanza kuharibika ili kuleta tija ya maendeleo

3 Ukarabati wa mradi wa maji ya Bomba-Duga Maforoni 26,000,000 21,674,284 Bwawa lina maji ya kutosha, lakini eneo hilo lipo wazi na hivyo kamati inashauri bwawa liimarishwe kwa kupanda miti kama vile mikuyu
4 Ujenzi wa darasa – shule ya Duga Maforoni 3,000,000 4,000,000 2,100,000 ili kumalizia jengo
Msisitizo uwekwe kuchangia kwa fedha ili kukamilisha mradi
5 Ujenzi wa ofisi ya kijiji cha Mtakuja 3,390,000 12,547,298 thamani ya jengo pamoja na choo haviendani na ‘value for money’. mfano, choo kilithaminishwa kwa gharama ya shilingi 2,950,000/= ambayo haiendani na hali halisi. Serikali ya kijiji itafute namna ya kumalizia ujenzi huo kutoka vyanzo vyake
6 Ujenzi wa darasa – shule ya msingi Maramba 5,607,000 4,665,200 Mradi huu ni mfano mzuri wa ‘value for money’ kwani kazi ni nzuri sana. Wanatakiwa kupewa kipau mbele kwa miradi mingine ijayo.Ofisi ya mkuu wa mkoa waliahidi kutoa kibali cha kupasua mbao za mlango, kuwekea dari na madawati.
7 Ujenzi wa nyumba ya mwalimu Daluni 3,600,000   Msingi wa nyumba upo chini sana na vyumba ni vidogo sana.
Kamati ilishauri Halmashauri isimamie nyumba hizi zijengwe kufuata ramani zilizotolewa Wizara
8 Ukarabati wa barabara ya Daluni – Kibaoni - Hemsambia km.6.3 13,480,000  

Katika ukaguzi huu hakukuwa na BOQ wala mtaalamu aliyetoa maelezo ya kina kuhusu ukarabati huo.

9 Ujenzi wa nyumba ya mwalimu shule ya msingi Hemsambia 3,600,000   Shule imepewa fedha tangu mwezi Machi 2008, na hadi wakati wa ukaguzi ilikuwa haijaanza kujengwa
wataalamu wa Halmashauri ya Mkinga waweke kambi shuleni kuhamasisha ujenzi wa nyumba ili ikamilike kwa wakati
10 Ujenzi wa ghala la mazao -Kata ya Maramba 36,000,000 29,600,000 Ghala hili litakuwa na umuhimu wa pekee kwa wananchi wa kata ya Maramba
Wananchi waandaliwe kwa kupata maelezo jinsi mazao yao yatakavyonunuliwa na kuhifadhiwa
 
HALMASHAURI YA WILAYA YA KILINDI
 
         
   

Kituo  cha  mabasi  Songe

Utekelezaji  upo  katika  hatua  za  mwisho,”cape  stones” zimeshawekwa,zimeshatumika  shilingi milioni  19  kati  ya  milioni  20  zilizotolewa.

Ushauri ulitolewa  Afisa  Mipango  wa  Wilaya Pangani kwa  uzoefu  aliokuwa  nao wakati  alipokuwa “Ubungo Bus Terminal” kwamba wafanye  marekebisho  katika ”cape  stones”zilizowekwa kulingana  na  idadi  ya  mabasi yanayoingia.

Walishauriwa  kuingiza  vifaa  katika  bajeti  yao  ili  kuharakisha  utendaji,

Ushauri  umetolewa  wakae na  kushauriana  kuanza  upya  na  kuingiza  katika  mpango  wa  ujenzi  wa  mradi  mwingine

Mhandisi  wa  wilaya  aangalie  kwa  makini  sehemu  iliyowekwa  zege  kwani  inaonyesha  kupitisha  maji.

Waharakishe  kumalizia “finishing’ ndogo ndogo ili watumishi  wahamie

 

 

Miti  ipandwe  na vyumba  vya  kilichokuwa  chuo cha  maendeleo  ya  wananchi viboleshwe.

 

Waharakishe  kujenga  vyoo ili boma  lianze  kutumika.

Ushauri ni  kwamba  h/mashauri  ipeleke  baadhi  ya  watumishi  Dar es Salaam  ili  kuangalia  mradi  wa  soko  la Temeke Sterio na Makumbusho jinsi wanalivyofanya.

   

Jengo  la  upasuaji  Songe

Jengo limeshakamilika,kumebaki umaliziaji  mdogo na kuingiza  vifaa  kama “operation table”  na  vingine

   

Wodi ya akina  mama Songe

Mradi  huu  ni  wa  miaka  ya  nyima,ujenzi  wake  haukufuata  ushauri  wa  kitaalam hivyo msingi  wake umepata “cracks” nyingi na imekuwa  vigumu  kuuendeleza.

   

Boma  la  Halmashauri

Mradi  huu  bado haujakmilika,wameshapandisha  kuta  na  kumwaga  zege  sehemu  ya  katikati.Awamu  ya  kwanza  walipokea  shilingi milioni 120 ambayo  ilitumika  katika  kufanya “consultation,design and  drawings” ambayo  ilipeleka  mradi  katika  “foundation level”,awamu  ya  pili  walipokea  shilingi  milioni 500 ambayo  ilipandisha  kuta.

   

Nyumba  za  watumishi

Mradi upo  katika  hatua  nzuri,umeezekwa  bado  kuweka  milango ili  watumishi  wahamie

   

Ofisi  ya  maji

Mradi umekamilika  na  baadhi  ya  ofisi  zimeshaanza  kutumika  kama  ofisi  ya  mhandisi  wa  maji  na mratibu  wa TASAF.Zimetumika  shilingi  milioni  52.Mradi  umetengewa  shilingi  milioni  10 mwaka  huu  wa  fedha  kwa  aijli  ya  samani

   

Mnada  wa  mifugo

Mradi  umekamilika,umegharimu  shilingi  milioni  45,ni mradi  wa ASDP   na LGCDG.

   

Shule  ya msingi-Mafisa  Majengo

Madarasa  3  yamekamilika  kwa  shilingi  milioni 29 pamoja  na  vifaa  vingine

   

Zahanati ya Kibirashi

Mradi  umefikia  hatu  nzuri, bado  kuwekwa  sakafu  na  kupakwa  rangi.

   

10.Ofisi  ya  kata

Boma  limefikia  hatua  ya  kuezekwa  bado  kuwekwa  mirango,sakafu  na vyoo  havijakamilika,mradi  umegharimu shilingi  milioni 9.

   

11.Soko  la  Kwediboma

Mradi  umefikia  hatua  nzuri.Bado  kuweka  vizimba,kiasi  cha  shilingi  milioni 44 zimetumika

 
 
HALMASHAURI YA WILAYA YA HANDENI
 
         
   

1.Kisima  cha  Minazini

Mradi  umeshakamilika  na  unatumika,unasambaza  maji  maeneo  ya magereza,hospitali  na  eneo  la Seuta

Wafanye  “compensation” ili kuongeza  eneo na  kuangalia  ‘contamination  ya  maji.

   

2.Tanki  la  maji Chanika

Mradi  umekamilika  na  unatumika

Mhandisi  aangalie “wash out’ ili  maji  yasituame  karibu  na  tanki.

   

3.Kituo  cha  mabasi Chogo

Mradi  unaetumika  ila  bado  haujakamilika  vizuri kama  upande wa  mifereji ya  kutolea  maji.

Mifereji  iwekwe  kulingana  na  hali halisi  ya  eneo

   

4.Shule  ya  Sekondari Handeni

Jengo  limeshaezekwa,bado ‘finishing’ nyingine

Mchanganyiko  wa  udongo  na seruji katika tofari uwe ni 1 kwa 10-12

   

5.Kisima  cha Kidereko

Kisima  kinatumika  ,wananchi  wanapata  maji

Waboreshe  mradi  ili  maji  yaweze  kwenda  juu  kwa  wananchi.

   

6.Shule  ya  Sekondari Kwamnyang’anyo

Mradi  umekamilika,wanafunzi  wameshaanza  kuingia  madarsani

Waongeze  matundu  ya  vyoo na kuweka  milango  chooni,wavune  maji  ya  mvua.

   

7. Shule  ya  Sekondari Kwaluguru

Ujenzi  wa  madarasa  2 umekamilika,ujenzi  wa  nyumba  ya  mwalimu  upo katika  hatua  ya  msingi

Wavune  maji  ya  mvua  kwa ajili  ya  kunywa  na  matumizi  mengine,waweke  wavu  katika  bomba  zinazotoa  hewa  nje  ili  kuzuia  nzi

   

8.Kisima kifupi  Kwachaga

Mradi  unatumika,wananchi  wanapata  maji  kwa  ‘pumping”

 

   

9.Soko  la  Suwa

Soko  limeshapauliwa ila  bado  halijaanza  kutumika.

Wakaangalie wenzao  wa  soko  la Kwediboma –Kilindi  walivyotekeleza  ili  wapate mifano.

   

10.Sekondari  ya Mazingira

Madarasa  3  yamekamilika,nyumba  ya  mwalimu  imekamilika  na  ameshahamia,bweni  la  wanafunzi  limekamilika  ila  bado  kuingiza  samani

Wataalamu  wa  maji  waangalie  uwezekano wa kuvuta  maji ya  bwawa  karibu  na  shule na wajenje  tanki  kubwa  la  kuifadhi  maji.

   

11.Soko  la  Mkata

Mradi  umekamilika pamoja  na  vyoo navyo  vimekamilika.Bado wafanyabiashara  hawajaanza  kuingia

Kuongeza “partition”ya vizimba ili  soko  kuchukua  idadi  kubwa.

   

12.Mradi wa maji Kwamnala

Mradi   haujakamilika  kutokana  na  kutokuepo  bwawa  karibu  na  tanki  lililojengwa.

Katika  vikao  vyao  waangalie  uwezekano  wa  kutumia  “resource”zilizowekwa  hapo ‘site”ili zitumike  katika  miradi mingine  kuhepuka  wizi  wa  hizo “resources” kama  mabomba

   

13Soko la Kwedizinga

Soko  limeshapauriwa,bado kuwekwa  sakafu.

Watanue  zaidi  vizimba  ili  kuchukua  idadi kubwa  ya  wafanyabiashara

   

14.Zahanati  ya Kwedizinga

Mradi  unatumika

Wavune  maji kukabiliana  ta  tatizo  la  maji

   

15.Umwagiliaji Masatu

Mradi  haujakamilika

Mradi  haujafuata  ushauri  wa  kitaalam,hivyo  wameshauriwa  kufuata  ushauri wa  kitaalam  na  baadae  wauombee fedha.

         
 
 
Title ya nyinginezo 2 [ Nyumbani ] au
Rudi juu
 
     
Copyright © 2008 - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Box 5095 Tanga, TEL: 027 - 2642430, FAX: 027-2647752