• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

AUSIMULIA MWENGE WA UHURU KUTOKA LAKI 3 HADI MILIONI 25 ZA UFUGAJI KUKU MKINGA

Imewekwa tarehe: June 16th, 2025

Na Mashaka Mgeta, MKINGA

WASWAHILI wanasema, ’mali bila daftari, hupotea bila habari.’ Lakini kwa Monica Kigoda, mkazi wa kijiji cha Duga Maforoni wilaya ya Mkinga mkoani Tanga, hali si hivyo.

Monica ametembelewa na Mwenge wa Uhuru 2025 leo Juni 15, 2025 kwenye eneo la mradi wa ufugaji kuku, akasimulia sehemu ya historia ya maisha yake tangu kuanza kwa biashara hiyo hadi sasa.

Akiwasilisha taarifa kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025, Ismail Ali Ussi, Monica amesema alianza biashara ya ufugaji kuku mwaka 2018 akiwa na mtaji wa Shilingi 300,000 iliyotokana na uuzaji wa mazao ya  kilimo cha bustani, ambapo alinunua vifaranga, dawa na chakula.

Akiwa amesimama mbele ya Mwenge wa Uhuru wenye ujumbe unaosema, JITOKEZE KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU WA 2025 KWA AMANI NA UTULIVU, Monica akasema biashara hiyo ilikuwa hatua kwa hatua, na kwa kufuata ushauri wa kitaalamu kutoka kwa Maafisa Biashara wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga, mtaji wake umekua hatua kwa hatua.

Monica anasema ukuaji wa mtaji umekuwa pamoja na ongezeko la idadi ya kuku anaowafuga, akitoa mfano kuwa alianza na kuku 100 , idadi hiyo ikaongezeka kufikia 800..

Kiongozi wa Mbio wa Mwenge wa Uhuru 20205, Ismail Ali Ussi, anasema Monica ni mfano wa kuigwa kwa uthubutu na ukuzaji wa biashara, hivyo anapaswa kuungwa mkono na wadau katika sekta za umma na binafsi.

Ussi amesema simulizi za Monica zimeonesha mapito ya ’milima na mabonde’, lakini akavumilia changamoto na sasa amekuwa na hadhi ya kufikiwa na Mwenge wa Uhuru 2025.

Kwa mujibu wa Ussi, vijana wanapaswa kutambua kuwa kazi za uzalishaji, huduma na ujasiriamali wanazoshiriki, zinathaminiwa sana nchini, kwa vile ni sehemu ya kutekeleza mang’amuzi ya Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa Watanzania kujitegemea na kuboresha maisha yao.

Ussi amesema hatua ya Monica kuwaajiri wakazi wengine wa Mkinga kushiriki biashara yake ya ufugaji kuku, ni sehemu ya uungwaji mkono na kumpa heshima Mhe Rais Dkt Samia.

”Monica, ulijitoa sana wakati ukinzisha ufugaji kuku kutokea nyumbani kwako, umestahimili changamoto nyingi ambazo sasa zinaondoka na unakuwa mwenye kuheshimika zaidi katika jamii yetu,” amesema Ussi.

Kiongozi wa Mwenge huyo, amesema itafaa sana ikiwa Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga itamuendeleza Monica kupitia mafunzo ya ndani na nje ya nchi, ili aweze kusambaza stadi za ufugajji kuku kwa Watanzania wengi zaidi.

.

 

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WAANDISHI DODOMA WAVUTIWA NA MAENDELEO YA TANGA, WAALIKWA KUFANYA ZIARA

    July 17, 2025
  • RC BATILDA:ONGEZEKO LA WATU TANGA ISHARA YA UBORA WA HUDUMA ZA FYA, USTAWI WA JAMII

    July 17, 2025
  • TANGA TUNA UTOSHELEZI WA CHAKULA - BALOZI BATILDA

    July 17, 2025
  • BALOZI BATILDA ASEMA TANGA INA HIFADHI YA LITA ZA UJAZO MILIONI 210 ZA MAFUTA

    July 17, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.