• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

HISTORIA YA UKOSEFU WA MAJI INAFUTWA MUHEZA

Imewekwa tarehe: May 19th, 2025


 

Na Mashaka Mgeta, MUHEZA

VIJIJI vitano vya wilayani Muheza katika Mkoa wa Tanga, yaani Kibanda, Mkinga, Tingeni, Mindu na Mbambata, vimekuwa kwenye kadhia ya ukosefu wa maji kwa muda mrefu.

Lakini sasa kero inaondoka, ikiwa ni ishara ya kufutika kwa historia ya ukosefu wa maji safi na salama, kufuatia visima virefu vinavyojengwa kwenye vijiji hivyo.

Kaimu Meneja wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) wilayani Muheza, Mhandisi Omary Mohamed, amesema hayo wakati akitoa taarifa kwa Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Tanga, ilipotembelea na kukagua miundombinu ya chanzo cha maji ya mradi huo kilichopo kijijini Mkinga.

Mhandisi Mohamed amesema ujenzi wa visima hivyo unaotarajiwa kukamilika Juni 30, mwaka huu, unatekelezwa kupitia kampuni za JNB Construction na Frangem International Limited.

Amesema mradi huo utagharimu Shilingi milioni 291.1, huku ukiwahudumia wakazi 3,950  waliopo kwenye maeneo ya mradi.

Kwa mujibu wa Mhandisi Mohamed, chanzo hicho kina urefu wa mita 160  kilichochimbwa majira ya kiangazi, kikiwa na uwezo wa kutoa lita mbili za maji kwa sekunde moja.

Amesema kutokana na uwezo huo, inachukua saa tano pekee kujaza tenki lililopo kwenye chanzo hicho, likiwa na ukubwa wa lita za ujazo 10,000 na uwezo wa kuwahudumiwa watu 800 kwa wakati mmoja.  

Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga, Mfaume Kizigo, ametoa rai kwa watendaji hasa katika ngazi za Serikali za Mitaa, kutumia vyombo vya habari kuujulisha umma mpana kuhusu miradi iliyopo kwenye maeneo yao na manufaa kwa maisha yao.

Amesema zipo habari njema nyingi zinazohusu utekelezaji wa miradi na maendeleo kwenye maeneo tofauti na ambazo haziifikii jamii ipasavyo, kutokana na ushirikishwaji mdogo wa waandishi na vyombo vya habari.

Kizigo amesema, pamoja na ukweli upataji habari zilizo sahihi na kweli ni haki ya kila raia, lakini hali hiyo inachochewa zaidi ya uwepo wa taarifa zinazohusu sekta zenye ‘kugusa’ maisha ya walio wengi.

 

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE)2023 January 25, 2024
  • HOTUBA YA MKUU WA MKOA WA TANGA MHE. WAZIRI WAZIRI KINDAMBA KATIKA HAFLA YA UFUNGUZI WA KONGAMANO LA UWEKEZAJI NA UZINDUZI WA MWONGOZO WA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOA WA TANGA 16/11/2023 November 27, 2023
  • FORM ONE SELECTION 2024 December 20, 2023
  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BILIONI 1.9 ZINAVYOIINGIZA TANGA KWENYE MALIPO YA KABLA YA MATUMIZI YA MAJI

    June 17, 2025
  • MWENGE WAONYA: MSIHARIBU MIUNDOMBINU, SERIKALI HAIJALALA

    June 17, 2025
  • RC BATILDA AZUNGUMZA MWENGE UKIHITIMISHA MBIO ZAKE TANGA

    June 17, 2025
  • MADAKTARI NA TUNU ZA UADILIFU KATIKA UTOAJI HUDUMA BORA KWA JAMII

    June 16, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.