• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

WATUMISHI WAELEKEZWA, JENGENI DESTURI YA KUZISOMA SHERIA NA KANUNI

Imewekwa tarehe: May 19th, 2025

Na Mashaka Mgeta, OMM TANGA

KATIBU Mkuu Ikulu, Mululi Mahendeka, amewataka watumishi wa umma kuzisoma, kuzielewa na kuzistafisiri kwa vitendo sheria, kanuni, taratibu na miongozo ya Serikali, ili kufanikisha utoaji huduma unaokidhi utatuzi wa kero za wananchi.

Mahendeka ameyasema hayo kwenye ufunguzi wa mafunzo ya siku tano yaliyoanza leo Mei 19, 2025 mjini hapa, yakiwashirikisha watumishi wa Idara za Rasilimaliwatu na Sheria kutoka taasisi 23 za Serikali, wanaohusika na masuala ya nidhamu za watumishi na kufanyia kazi malalamiko ya wananchi.  

Lengo la mafunzo hayo ni kukumbushana na kueleweshana uzingatiaji wa sheria, kanuni na taratibu katika utekelezaji wa majukumu ya watumishi, hasa kwenye usimamizi na uendeshaji wa mashauri ya nidhamu, malalamiko, rufaa na kero za watumishi na wananchi wengine.

Hotuba yake kwenye mafunzo hayo yaliyoandaliwa na Ofisi ya Rais, Ikulu kwa kushirikisha Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Tume ya Utumishi wa Umma, imesomwa kwa niaba yake na Katibu Tawala Mkoa wa Tanga, Pili Mnyema.

Mahendeka amesema, kwa  kufanya hivyo jamii itanufaika kwa usimamizi na uendeshaji wa mashauri ya nidhamu, malalamiko, rufaa na kero za watumishi wa umma na wananchi kufanyika kwa haraka, ukamilifu na kupatiwa ufumbuzi.

Pili ni kuwaondolea wananchi na watumishi wa umma usumbufu wa kufuatilia majibu ya malalamiko, kero kwenye mamlaka za juu kama vile kwa Mhe Rais, Mhe Makamu wa Rais, Mhe Waziri Mkuu, Katibu Mkuu Kiongozi na viongozi wengineo.

Tatu, kuepuka gharama ambazo Serikali inaweza kulipa, endapo imeshindwa kesi inayotokana na suala la hatua za kinidhamu, zilizochukuliwa kwa mtumishi wa umma au mwenye madai dhidi ya Serikali.

Nne, kuepusha wananchi wakiwemo watumishi wa Serikali, kuichukia Serikali pale ambapo hawakuhudumiwa vizuri au malalamiko, kero zao hazikutatuliwa kwa wakati.  

Kero za wananchi ama watumishi zinapofanyiwa kazi kwa haraka na wakati, zinafanya waiamini zaidi Serikali na kushiriki ipasavyo katika shughuli za maendeleo.

Tano, kuepusha viongozi wakuu wa nchi kutumia muda mwingi kusikiliza malalamiko, kero za wananchi na kuzitatua, wakaati wana majukumu mengi kwa maendeleo ya kijamii, kiuchumi na kisiasa.

Matangazo

  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • SENSA YA WATU NA MAKAZI MWAKA 2022 MKOA WA TANGA June 13, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • VIJANA PANGANI 'WAKOSHWA' NA MIKOPO YA ASILIMIA 10

    November 27, 2025
  • BOMBO YAZINDUA WODI BINAFSI KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA TANGA

    November 27, 2025
  • EACOP YAELEZA MAENDELEO YA MRADI WA BOMBA LA MAFUTA GHAFI

    November 25, 2025
  • GCUs WATAKIWA KUTUMIA HABARI KUCHAGIZA TABASAMU KWA WATANZANIA

    November 21, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.