• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

MATOKEO YA KIDATO CHA SITA, MAPATO ‘YANAVYOMGUSA’ RC TANGA

Imewekwa tarehe: July 16th, 2024

Na Mashaka Mgeta, OMM-TANGA

 

UPO usemi unaosema, ‘’mtu anapofanya jambo la kusifiwa, sharti asifiwe’’. Ndivyo inavyotamkwa na Mkuu wa Wilaya ya Kilindi, Mhe Hashim Mgandilwa kwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe Balozi Dk Batilda Burian.

 

Mhe Mgandilwa anayesema hayo kufuatia ‘kuguswa’ na mafanikio ya mkoa huo katika sekta ya elimu na ukusanyaji mapato ya ndani, kwamba vimechochewa na usimamizi, ufuatiliaji na maelekezo ya Mhe Balozi Dk Batilda.

 

Anasema hayo leo Julai 16, 2024, baada ya Mhe Balozi Dk Batilda, kuelezea furaha yake kwa matokeo mazuri katika sekta hizo.

 

Akizungumza kwenye halfa ya kukabidhi magari manne kwa Wakuu wa Wilaya tatu na Mkuu wa Idara ya Mipango katika Sekretarieti ya Mkoa huo, Mhe Balozi Dk Batilda, amesema matokeo ya kidato cha sita yanayoonesha mkoa huo kujitokeza kwenye ‘kumi bora’, kunatia moyo wa kuzidi kukuza kiu ya kuiboresha zaidi sekta hiyo.

 

Kwa mujibu wa Mhe Balozi Dk Burian, Shule ya Sekondari ya Mkindi na wasichana waliofanya vizuri kwenye ‘kumi bora’  kitaifa, ni ishara kwamba upo uwezekano kwa mkoa huo kufanya vizuri zaidi kwenye maeneo hayo.

 

‘’Kwa vile historia inaonyesha hapa Tanga ndipo elimu ilipoanzia nchini, hatujaridhika na mafanikio ya mwaka huu, tunajipanga kufanya vizuri zaidi,’’ amesema.

 

Mhe Balozi Dk Burian amesema, pamoja na mafanikio hayo, jitihada za uboreshaji wa sekta ya elimu, unachochewa pia na hatua ya Mhe Rais Dk Samia Suluhu Hassan, kuwekeza fedha nyingi mkoani humo.

 

Amesema miongoni mwa fedha hizo ni Shilingi bilioni 3 zilizotumika kujenga Shule Maalum ya Wasichana ya Mkoa wa Tanga iliyopo Mabalanga wilayani Kilindi, sasa imewapokea kwa mara ya kwanza wanafunzi wa kidato cha tano mwaka huu.

 

Mhe Balozi Dk Burian amesema, serikali imetoa fedha nyingine, Shilingi bilioni 1.1 kuendeleza ujenzi wa miundombinu shuleni hapo.

 

Mhe Balozi Dk Burian, amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Kilindi, Mhe Mgandilwa kuongeza ufuatiliaji, usimamizi na ukaguzi wa ujenzi wa shule hiyo.

 

Kuhusu mapato ya ndani kwa mwaka 2023/2024, Mhe Balozi Batilda amesema hatua ya kufikia asilimia 104 inaonesha uwezekano wa kukusanya mapato zaidi mkoani humo.

 

Takwimu za makusanyo hayo na asilimia ya malengo kwa kila halmashauri kwenye mabano ni Kilindi (131), Mji Handeni (128), halmashauri ya wilaya Handeni (125), Muheza (108) na Bumburi (102).

 

Halmashauri nyingine ni jiji la Tanga, Mkinga na Lushoto zilizofikisha asilimia 98 kila moja, halmashauri ya wilaya Korogwe (97), Mji Korogwe (93) na Pangani (95).

 

Hapo ndipo Mhe Mgandilwa anasema, mafanikio hayo hayawezi kuweka kando nafasi ya maelekezo, ufuatiliaji na usimamizi wa Mhe Balozi Dk Burian, kupitia Sekretarieti ya Mkoa inayoongozwa na Katibu Tawala Mkoa, Pili Mnyema.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE)2023 January 25, 2024
  • HOTUBA YA MKUU WA MKOA WA TANGA MHE. WAZIRI WAZIRI KINDAMBA KATIKA HAFLA YA UFUNGUZI WA KONGAMANO LA UWEKEZAJI NA UZINDUZI WA MWONGOZO WA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOA WA TANGA 16/11/2023 November 27, 2023
  • FORM ONE SELECTION 2024 December 20, 2023
  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BILIONI 1.9 ZINAVYOIINGIZA TANGA KWENYE MALIPO YA KABLA YA MATUMIZI YA MAJI

    June 17, 2025
  • MWENGE WAONYA: MSIHARIBU MIUNDOMBINU, SERIKALI HAIJALALA

    June 17, 2025
  • RC BATILDA AZUNGUMZA MWENGE UKIHITIMISHA MBIO ZAKE TANGA

    June 17, 2025
  • MADAKTARI NA TUNU ZA UADILIFU KATIKA UTOAJI HUDUMA BORA KWA JAMII

    June 16, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.