• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

MILIONI 100 ZATOLEWA KUBORESHA SOKO LA NGAMIANI TANGA

Imewekwa tarehe: April 26th, 2025


Na Mashaka Mgeta, OMM TANGA

HALMASHAURI ya Jiji la Tanga imetenga na kutoa Shilingi milioni 100 kwa ajili ya uboreshaji wa soko kongwe la Ngamiani, ili kuweka mazingira yenye staha kwa wafanyabiashara na wateja wake.

Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Lusajo Gwakisa, amesema hayo alipotoa taarifa kwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe Balozi Dkt Batilda Burian, aliyefanya ziara ya ghafla leo asubuhi, kufuatia kusambaa kwa picha mjongeo ikionyesha sehemu za soko hilo kuvuja maji yanayotokana na mvua zinazonyesha.

Gwakisa amesema uboreshaji wa soko hilo unatekelezwa na mkandarasi aliyeshinda zabuni ya kazi hiyo, kampuni ya Ms Spacetec Corporatioon Limited.

Kwa mujibu wa Gwakisa, uboreshaji wa soko hilo ulioanza, ulisitishwa kutokana na ombi la wafanyabiashara waliotaka usitishwe ili wafanye biashara katika kipindi cha sikukuu za Idd el Fitr na Pasaka.

“Baada ta sikukuu hizo, zilianza kunyesha mvua zilizosababisha maeneo tuliyokusudia kuyaboresha, yakavujisha maji kama ilivyochukuliwa kwenye picha mjongeo iliyosambazwa kupitia mitandao ya kijamii,” amesema.

Hoja hiyo imeungwa mkono na Mwenyekiti wa Wafanyabiashara wa Soko la Ngamiani, Shaban Ramadhan aliyesema wanashirikiana na uongozi wa jijini la Tanga kukabiliana na changamoto zilizopo ikiwemo maeneo yanayovuja.

Ramadhan amesema picha mjongeo iliyorushwa kwenye mitandao ya kijamii, ‘imebeba’ ujumbe wa sauti wenye kupotosha kutokana na shutuma zinazotolewa kwa lengo la kuuaminisha umma kwamba hakuna jitihada zinazofanyika, jambo ambalo si kweli.

Mmoja wa wafanyabiashara sokoni hapo, Jonathan Mpanduka, amekemea hatua ya watu wasiokuwa na nia njema, kupiga na kusambaza picha zinazopotosha ukweli unahusu changamoto zilizopo kwenye soko la Ngamiani na namna Serikali inavyozitatua kwa kushirikiana nao (wafanyabiashara).

Kaimu Mhandisi wa Jiji la Tanga, Jumaa Jumanne, amesema miongoni mwa kazi zinazofanyika katika ukarabati wa soko hilo ni  kuboresha mifereji yam aji machafu, kuondoa bati na ‘gata’ chakavu na kuweka mpya.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe Balozi Dkt Batilda Burian, amemuagiza Mkurugenzi wa Jiji la Tanga kushirikiana na Mkandarasi huyo, kubuni namna bora ya kutekeleza ukarabati wa soko hilo pasipo kuwaondoa wafanyabiashara.

Pia, Mhe Dkt Batilda amesema, ukarabati huo unapaswa kufanyika kwa kasi ili ukamilike haraka, ikibidi kuongeza nguvu kazi zaidi ya inayotumika sasa.

Mhe Balozi Dkt Batilda amesema mazingira bora kwa wafanyabiashara na watumiaji wa masoko ya bidhaa mbalimbali, ni miongoni mwa vipaumbele vya Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, hivyo kuwahikikishia (wafanyabiashara wa Ngamiani) kwamba changamoto zinatatuliwa ndani ya muda mfupi.

Pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Jiji, Mhe Balozi Dkt Batilda alifuatana na Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Mhe Japhari Kubecha na Katibu Tawala Wilaya (DAS), Dalmia Mikaya.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE)2023 January 25, 2024
  • HOTUBA YA MKUU WA MKOA WA TANGA MHE. WAZIRI WAZIRI KINDAMBA KATIKA HAFLA YA UFUNGUZI WA KONGAMANO LA UWEKEZAJI NA UZINDUZI WA MWONGOZO WA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOA WA TANGA 16/11/2023 November 27, 2023
  • FORM ONE SELECTION 2024 December 20, 2023
  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • TANGA 'YAITIKA' WAZIRI MCHENGERWA AKIWAITA MAAFISA HABARI WA MIKOA, HALMASHAURI DODOMA

    May 21, 2025
  • KATIBU MKUU IKULU AFUNGUKA NA KUWAELEKEZA WATUMISHI WASIKIUKE MAADILI

    May 20, 2025
  • WATUMISHI WAELEKEZWA, JENGENI DESTURI YA KUZISOMA SHERIA NA KANUNI

    May 19, 2025
  • HISTORIA YA UKOSEFU WA MAJI INAFUTWA MUHEZA

    May 19, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.