• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

SPIKA BWZ ATEMBELEA MIRADI YA BILIONI 8 TANGA

Imewekwa tarehe: April 26th, 2025


Na Mashaka Mgeta, OMM TANGA                 

SPIKA wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar (BWZ), Mhe Zubeir Ali Maulid leo Aprili 25, 2025 ametembelea miradi ya maendeleo katika sekta za elimu na uchumi, yenye thamani ya takribani Shilingi bilioni 7.4 mkoani Tanga.

Mhe Maulid yupo mkoani humo kwa ziara ya siku nne iliyoanza jana, ikiwa ni sehemu ya shamrashamra za maadhimisho ya miaka 61 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar uliofikiwa Aprili 26, 1964.

Mradi wa kwanza ulikuwa ujenzi wa madarasa manne ya kidato cha tano na sit ana matundu saba ya vyoo kwenye Shule ya Sekondari Bushiri wilayani Pangani ulioanza Januari 25, 2024 na kugharimu Shilingi milioni 116.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Pangani, Charles Fussi, amesema kukamilika kwa mradi huo kutawanufaisha wanafunzi wanaohitimu kidato cha nne kupata nafasi zaidi za kujiunga kidato cha tano, na kuongeza hamasa ya kuthamini elimu. 

Aidha, Mhe Maulid alitembelea mradi wa ujenzi wa mabweni mawili ya wanafunzi wa kidato cha tano na sita katika Shule ya Sekondari Zingibari wilayani Mkinga, unaogharimu Shilingi milioni 260.

Mkuu wa shule hiyo, Mwalimu Omar Rashid, amesema mradi huo uliibuliwa ili kutatua changamoto ya upungufu wa mabweni kwa wanafunzi wa kidato cha tano na sita ili kuisaidia jamii ya wanafunzi kuwa salama na kuongeza ufaulu.

Pia Mhe Maulid, ametembea mradi wa ujenzi wa miundombinu ya soko la wafanyabiashara wadogo kwenye eneo la Kange jijini Tanga ambao hadi kukamilika kwake, utakaogharimu Shilingi bilioni 7.7.

Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Tanga, Gwakisa Lusajo amesema ujenzi wa soko hilo utafanyika kwa awamu nne na inakisiwa, kila awamu itagharimu Shilingi bilioni 1.9, lengo likiwa ni kukidhi mahitaji ya wafanyabiashara wadogo.

Spika wa BWZ, Mhe Maulid amesema miradi hiyo na mingine iliyopo sehemu nyingine za mkoa huo na nchini, ni sehemu ya vilelezo vya namna Serikali ya Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, inavyotekeleza kwa vitendo Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya 2020 hadi 2025.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe Dkt Batilda Burian, amesema ufanisi katika utekelezaji wa miradi mkoani humo, unachochewa na ushirikiano mzuri uliopo kati ya Serikali, Chama tawala na wananchi.


 

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE)2023 January 25, 2024
  • HOTUBA YA MKUU WA MKOA WA TANGA MHE. WAZIRI WAZIRI KINDAMBA KATIKA HAFLA YA UFUNGUZI WA KONGAMANO LA UWEKEZAJI NA UZINDUZI WA MWONGOZO WA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOA WA TANGA 16/11/2023 November 27, 2023
  • FORM ONE SELECTION 2024 December 20, 2023
  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • TANGA 'YAITIKA' WAZIRI MCHENGERWA AKIWAITA MAAFISA HABARI WA MIKOA, HALMASHAURI DODOMA

    May 21, 2025
  • KATIBU MKUU IKULU AFUNGUKA NA KUWAELEKEZA WATUMISHI WASIKIUKE MAADILI

    May 20, 2025
  • WATUMISHI WAELEKEZWA, JENGENI DESTURI YA KUZISOMA SHERIA NA KANUNI

    May 19, 2025
  • HISTORIA YA UKOSEFU WA MAJI INAFUTWA MUHEZA

    May 19, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.