• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
Tanga Region
Tanga Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Tanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhima
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za maji
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango na Uratibu
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Afya
      • Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Usimamizi wa Serikali za Mitaa
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa ndani
      • Manunuzi
      • Sheria
  • Machapisho
    • Taratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Hotuba
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Sehemu ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya Pangani
    • Halmashauri ya Wilaya Mkinga
    • Halmashauri ya Wilaya Muheza
    • Halmashauri ya Jiji Tanga
    • Halmashauri ya Wilaya Korogwe
    • Halmashauri ya Mji Korogwe
    • Halmashauri ya Wilaya Handeni
    • Halmashauri ya Mji Handeni
    • Halmashauri ya Wilaya Kilindi
    • Halmashauri ya Wilaya Lushoto

TANGA 'YAITIKA' WAZIRI MCHENGERWA AKIWAITA MAAFISA HABARI WA MIKOA, HALMASHAURI DODOMA

Imewekwa tarehe: May 21st, 2025


Na Mashaka Mgeta, OMM TANGA

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi),  Mhe Mohamed Mchengerwa, atakutana na Maafisa Mawasiliano wa Sekretarieti za Mikoa na Maafisa Habari wa Halmashauri nchini Mei 23 na 24, mwaka huu.

Kikao hicho cha mafundo na mazingativu, kitafanyika jijini Dodoma, lengo likiwa ni kuongeza ufanisi kiutendaji kwa maafisa hao.

Taarifa ya TAMISEMI imeeleza, kupitia kikao hicho, utawekwa mkakati endelevu wa kuhabarisha umma kuhusu hatua mbalimbali za maendeleo ya nchi, hususani katika uongozi wa Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Maafisa hao wamekuwa kiunganishi bora kati ya wananchi na Serikali, na kupasha habari za Serikali kuhusu utekelezaji wa majukumu yake.

Pia taarifa hiyo ya TAMISEMI imesema Maafisa Mawasiliano na Habari wa Serikali, wamefanikisha kuuhabarisha umma kuhusu mafanikio na changamoto na kupaza sauti za wananchi.

Katibu Tawala Mkoa wa Tanga, Pili Mnyema, amesema kikao hicho kwa kada hiyo ni muhimu sana hasa kwa wakati huu kunapohitajika nguvu za kuboresha na kuimarisha zaid mawasiliano na kati ya Serikali na wananchi.

Mnyema ameshawaelekeza Wakurugenzi wa halmashauri 11 za mkoni humo, kuwawezesha Maafisa Habari wao kushiriki kikao hicho kwa ufanisi.

”Sisi (Tanga) hatuna mzaha katika utekelezaji wa maelekezo ya Serikali, tunatambua umuhimu wa kikao hiki na mwaliko wa Mhe Waziri ni maelekezo, hivyo kila halmashauri itamuwezesha Afisa Habari wake kushiriki,” amesema.

Maafisa Habari wa mkoani humo, wameelezea kupata muitikio mzuri wa Wakurugenzi wao, na wana imani ushiriki katika kikao kazi hicho utaongeza chachu yenye kuleta matokeo chanya katika utendaji kazi wao, halmashauri na mkoa wa Tanga.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE)2023 January 25, 2024
  • HOTUBA YA MKUU WA MKOA WA TANGA MHE. WAZIRI WAZIRI KINDAMBA KATIKA HAFLA YA UFUNGUZI WA KONGAMANO LA UWEKEZAJI NA UZINDUZI WA MWONGOZO WA FURSA ZA UWEKEZAJI MKOA WA TANGA 16/11/2023 November 27, 2023
  • FORM ONE SELECTION 2024 December 20, 2023
  • TANGA REGION INVESTMENT GUIDE November 24, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BILIONI 1.9 ZINAVYOIINGIZA TANGA KWENYE MALIPO YA KABLA YA MATUMIZI YA MAJI

    June 17, 2025
  • MWENGE WAONYA: MSIHARIBU MIUNDOMBINU, SERIKALI HAIJALALA

    June 17, 2025
  • RC BATILDA AZUNGUMZA MWENGE UKIHITIMISHA MBIO ZAKE TANGA

    June 17, 2025
  • MADAKTARI NA TUNU ZA UADILIFU KATIKA UTOAJI HUDUMA BORA KWA JAMII

    June 16, 2025
  • Angalia zote

Video

KATIBU TAWALA MKOA WA TANGA AKIONGOZA WATUMISHI WA MKOA HUO KUFANYA MAZOEZI YA PAMOJA KATIKA UWANJA WA MKWAKWANI KUITIKIA WITO WA MHE. MAKAMU WA RAIS
Video zaidi

Viunganishi vya haraka

Tovuti zinazoendana

  • TAMISEMI
  • Kupata huduma za kiutumishi
  • Wakala ya Serikali Mtandao
  • Utumishi
  • Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)
  • Tovuti ya Serikali

Kifuatilia watazamaji duniani

world map hits counter

idadi ya watazamaji

free HitCounter

Ramani ya Mkoa wa Tanga

Wasiliana nasi

    Golf Area/Masiwani Road Tanga

    Anuani ya posta: P.O.Box 5095 Tanga

    Simu: 027 2642421

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ras.tanga@tamisemi.go.tz

Anuani zingine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki miliki ©2017 Katibu Tawala Mkoa wa Tanga . Haki zote zimehifadhiwa.